Dec 27, 2013

HIVI NDIVYO LIVYOKUWA SIKU YA CHRISTMAS PANDE ZA KAHAMA TENGUA KAULI NA BROTHER K WA FUTUHI




Hii ilikuwa ni jana mchana katika viwanja vya Masabo mjini Kahama ambapo walikuwepo Brother K na sharobaro wa Kihaya kutoka FUTUHI ya Star TV Pamoja na Chili na Ringo kutoka Vituko show ya Chanel Ten.

Show hii imeandaliwa na redio kahama FM, na kuwashirikisha watoto pamoja na watu wazima yani show ya kifamilia zaidi.

Umati wa watu walioshuhudia show hiyo
Moja kati ya Mchezo waliouonesha wote kwa pamoja
Wadau wa Kahama fm wakiangalia show
Kulikuwa na nyomi si mchezo
Brother K, Chili na Sharo la kihaya
Chili aliyekaa na Ringo anayevizia kwa pembeni wakifanya yao

Pombe noumaa!!! KONYAGI YAUA MFANYAKAZI WA TIGO SIKU YA KRISMASI...!!


Mwanamme aitwayeGodi Shaini Fanuel Mangala (34)  mkazi wa mtaa wa Majengo Mapya  kata ya Ngokolo mjini Shinyanga amefariki dunia kwa kile kinachosadikiwa kuwa ni kunywa
pombe aina ya konyagi kupita kiasi.

Mashuhuda wa tukio hilo wameimbia malunde blog kuwa tukio hilo la kusikitisha limetokea siku ya krismasi  Desemba 25 mwaka huu saa moja jioni.

Wamesema marehemu alikuwa anakunywa pombe na wenzake katika  moja ya Glosary mjini Shinyanga na  baadaye mwenzao alizidiwa na kulazimika kurudishwa nyumbani kwake ili akapumzike na hali ilipozidi  kuwa mbaya wakampeleka katika hospitali ya mkoa lakini akafariki dunia akiwa njiani

Hata hivyo mmoja wa  mashuhuda hao ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kabla ya kifo hicho marehemu alikuwa anashindana na wenzake kunywa pombe maarufu konyagi ama wengine wanapenda kuziita Bapa.

Diwani wa kata ya Ngokolo mjini Shinyanga kulikotokea tukio hilo Sebastian Peter amesema kifo cha God ni mipango ya mungu kutokana na kwamba marehemu hakuwa mgeni wa pombe na kwamba inadaiwa kuwa kabla ya kifo hicho marehemu alikuwa analalamika kusumbuliwa na vichomi siku hiyo.

Akizumgumzia tukio hilo mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt Fredrick Mlekwa alikiri kuupokea mwili  wa marehemu muda wa saa moja jioni Desemba 25 mwaka huu,akiwa tayari amefariki dunia na kesho yake Desemba 26 ndugu wa marehemu walifika hospitalini hapo na kuuchukua mwili wa marehemu kwa ajili ya mazishi hivyo kushindwa kufanya uchunguzi wa kitaalamu ili kubaini chanzo cha kifo hicho.
 
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga SACP Evarist Mangala amesema bado hajapata taarifa kuhusu tukio hilo.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa rafiki wa karibu na marehemu anayejulikana kwa jina la John tayari mwili wa marehemu God Shaini umesafirishwa kwa ajili ya mazishi hapo kesho nyumbani kwa mama yake  Mabatini mkoani Mwanza.

"Mkorogo Umenitia Adabu sana"...Wema Sepetu..!!


MISS Tanzania 2006 aliye pia staa wa filamu za Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ amevunja ukimya kwa kuweka wazi kuwa, mkorogo umemtia adabu na anajuta kuutumia  mwilini mwake.
Wema Sepetu
Akizungumza juzi na paparazi wetu ofisini kwake jijini Dar, Wema alisema  kuwa baada ya kwenda kliniki nchini China na kupata matatibu ya ngozi yake ambayo sasa imerudi kama mwanzo amejifunza kitu.

NI KITU GANI HICHO?
Wema alisema amejifunza kuwa, binadamu anatakiwa kuishi alivyoumbwa na Mungu, mambo ya rangi ya mwili hayana nafasi katika uwezo wa binadamu.

ALIAMINI USTAA NI LAZIMA UWE MWEUPE PEE!
Wema akatoa mpya zaidi aliposema kuwa, uamuzi wake wa kutumia mkorogo ili awe mweupe kama mzungu (yeye ni mweupe) ulitokana na kuamini kwamba, weupe na ustaa ni mambo yanayokwenda pamoja, kumbe sivyo.

Niliamini weupe sana na ustaa ni Kulwa na Doto, lakini sivyo. Ngozi yangu ya awali ni nzuri, imerudi kama ilivyokuwa, namshukuru sana Mungu,” alisema Wema.

AWAONYA MASTAA WENZAKE
Akiendelea kuzungumza na paparazi, Wema alitoa ujumbe kwa mastaa wenzake wanaotumia mkorogo kuwa, hakuna faida yoyote, kwa sababu mkorogo unaondoa vitamini yote mwilini.

Daktari kule China aliniambia kuwa licha ya kupoteza vitamini nyingi mwilini, pia mkorogo unakufanya mtu uzeeke kabla ya  wakati. Mimi nawaomba kabisa mastaa wenzangu wajiepushe na hii kitu inaitwa mkorogo,” alisema Wema.

ALICHOJIFUNZA KUHUSU KUJIKOBOA
Kujikoboa ni kuwa mweupe sana, lakini Wema anasema alichojifunza kuhusu hali hiyo ni kwamba, ni rahisi sana kuiondoa ngozi ya awali kwa mkorogo lakini inapofika ngozi ya awali inatakiwa kurudi inagharimu sana.

Ukitaka kuona maajabu sasa, ngozi yako mwenyewe kuibadilisha si kazi na wala si gharama lakini ukitaka irudi kama mwanzo ni lazima ugharimike sana, mimi sitaki tena jamani,” alisema Wema.

Jul 10, 2013

ZITTO KABWE AWATAKA WANANCHI WAGOME KUILIPA KODI YA SIMU YA SH. 1000.....AMEDAI KUWA KODI HIYO ILIPITISHWA KINYEMELA



Sakata  la  kodi  ya  line  ya  simu  limeendelea  kuwakuna wanasiasa  wetu  ambao  wamekuwa  wakifunguka  kwa  nyakati  mbalimbali  kupitia mitandao  ya  kijamii....

Baada  ya  January  Makamba, Zitto  kabwe  naye  amefunguka  na  kudai  kuwa  kodi  hiyo  ni  batili  na  ilipitishwa  kinyemela  kwa  sababu  ilikuwa  imeshaondolewa....

Huu  ni  ujumbe  wake  aliouweka  katika  account  yake  ya  facebook:
Baada ya  kauli  hiyo,Zitto  Kabwe  aliandamwa  na  maswali  mengi  sana  toka  kwa  wananchi  wakidai  kuwa  "Makamba  alisema  tuwalaumu  ninyi  maana  ninyi  wabunge  ndo  mlibariki  kodi  hii"

Zitto  naye  alishindwa  kulijibu  swali  hilo  na  kuwataka  wananchi  "wachukue  simu  zao, wawapigie  wabunge  wao  wawaulize  ni  kwa  nini  walipitisha  kodi  hii"

 "Anasema  hiyo  kwa  sababu  wabunge  ndio waliopitisha.Wabunge  ndio  wawakilishi  wa  wananchi.Jambo likipita bungeni hao ndio wa kwanza kulaumiwa.Yupo sahihi kabisa.Mpigie mbunge wako simu muulize kwa nini  alikubali au  hakupinga kodi hii"..Hili  ni  jibu  za  Zitto Kabwe

JANUARY MAKAMBA AWATAKA WANANCHI WAWALAU WABUNGE WAO KUHUSU KODI YA 1000 KWA KILA LAINI.....ADAI WIZARA YAKE ILIPINGA VIKALI



Haya  ni  majibu ya  Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. January Makamba akijibu maswali katika mtandao wa Twitter kuhusu kodi mpya ya TZS 1000 kwa mwezi kwa kila line ya simu. 


  •  Amesema kwamba Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia iliipinga kodi hiyo.

  •  Amesema kwamba Hazina (Wizara ya Fedha) walikubaliana na maoni ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kuhusu kodi hiyo.
  • Amesema kwamba Bunge ndilo lililopitisha kodi hiyo na si Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.

"NITAENDELEA KUPAMBANA NA WABISHI WASIOTAKA KUHAMA ILI KUPISHA MIRADI YA UJENZI"...MAGUFULI



WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli ameapa kupambana kwa kuwabomolea au kuwakomesha kwa njia nyingine, watu waliogoma kuhama kwa ajili ya kupisha miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na wizara yake.

Katika hilo, tayari amekwishatangaza uamuzi mzito wa kuruhusu kampuni ya ujenzi ya Jaspal Singh, kujenga barabara kwa kiwango cha lami kwa kuzizunguka nyumba za wakazi waliogoma kuhama na kukimbilia mahakamani akiamini kuwa wataondolewa kwa kugongwa na malori yatakayokuwa yakipita baada ya barabara hiyo kukamilika.

Pamoja na hilo, Dk. Magufuli amesema atazibomoa bila kulipa fidia nyumba za wananchi nane waliokataa kufanyiwa tathmini ili kupisha mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni, endapo hawatabadili msimamo wao huo.

Uamuzi huo aliutangaza jana baada ya kufanya ziara ya kutembelea miradi mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam, ambapo alibaini kuwa miradi mingi inakwamishwa na wananchi wa maeneo husika.

Akiwa katika mradi wa ujenzi wa barabara ya Kigogo hadi Jangwani yenye kilomita 2.7, alishangazwa kuona mradi umesimama huku vifaa vikionekana kuwa na kutu kitendo ambacho kilimlazimisha ahoji.

Mhandisi Mshauri wa mradi huo, Mussa Ali pamoja na Mkandarasi Jaspal Hungh, walimueleza Magufuli kwamba kuna wananchi wenye nyumba 16 wamechukua fidia na kufungua kesi mahakamani kwa kudai kiasi walichopewa ni kidogo.

Aliongeza kuwa kesi hiyo imechukua zaidi ya miaka miwili bila kutolewa hukumu na kusababisha mradi kukwama.

TAMKO LA KIGOGO

Akizungumzia hilo Magufuli alisema: “Naomba tusiingilie mahakama lakini naagiza kuanzia leo (jana), anzeni kujenga barabara ya lami kwa kuzizungushia lami nyumba hizo na kuruhusu gari zipite, nadhani haitapita wiki kabla hazijagongwa na malori ya mchanga, sitaki kusikia Serikali inadaiwa fidia ya ucheleweshaji wa mradi.

“Pia naagiza kwamba mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki kwamba meneja wa mradi fungua kesi dhidi ya wananchi hao waliochukua fedha za fidia na kwenda mahakamani, huo ni wizi.

“Serikali ikishinda kesi ya madai yao ya fidia ndogo, wao ndio watawajibika kujenga sehemu ya nyumba zao, hatuwezi kuchezea fedha kwani kuwafidia Sh bilioni 3.8 ambapo mradi wenyewe unagharimu Sh bilioni 7.6.

“Kuna mazoea yameibuka ya watu kuchezea Serikali na mahakama, sasa nasema katika miradi ya wizara yangu nitapambana nao watu wenye kiburi cha kuchezea vyombo hivyo,” alisema.

DARAJA L A KIGAMBONI

Awali akitembelea eneo la Kigamboni uliko mradi wa daraja la Kigamboni, Magufuli aliwataka wananchi nane waliokataa kufanyiwa tathmini ya nyumba zao ili kupisha mradi huo, kubadili msimamo wao haraka kabla ya Serikali haijazibomoa nyumba hizo kwa nguvu tena bila kulipwa.

Jumla ya watu 121 walitakiwa kuhama kupisha mradi huo ambapo kati yao 113 walikubali kufanyiwa tathmini na kulipwa jumla ya Sh bilioni 11.7, lakini nane walikataa.

“Nasema Serikali ikiamua kufanya ukorofi utakuwa mkubwa kuliko msimamo wako, sasa nasema hao waliokataa kufidiwa naomba wasiambulie patupu kabla hatua hazijachukuliwa, wakubali kuchukua kiasi kitakachothaminiwa haraka, sisi tukija tutabomoa na hatukulipi na mradi utaendelea.

“Naomba daraja hili likamilike na kukabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete Januari 31, 2015 na kulifungua, sitaki kuona linafunguliwa na rais mwingine ambaye anaweza kusema yeye ndiye aliyejenga wakati ni uongo, aliyeweka jiwe la msingi ndiye atakayefungua,” alisema.

Mradi wa daraja la Kigamboni unagharimu Sh bilioni 214 na kati hizo asilimia 40 zinatolewa na Serikali wakati Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), unachangia asilimia 60.

Mbali na hilo, Dk. Magufuli ameagiza kuondolewa haraka wakazi wa eneo la Davis Corner, Temeke ambao licha ya kulipwa fidia ili kupisha ujenzi wa barabara ya Jet Corner hadi Temeke, wameshindwa kuhama mpaka sasa na badala yake kutumia fedha hizo kuendeleza ujenzi na kudai malipo mengine.

Magufuli alishangazwa kuona wananchi hao ambao wamegoma hadi sasa wamelipwa fidia Sh 15.8 huku mradi wenyewe ukiwa Sh bilioni 12 na barabara ikiwa haijakamilika.

Mradi wa mabasi ya kasi

Akikagua mradi wa mabasi yaendayo kasi jijini Dar es Salaam (DARTS), Magufuli alifurahishwa na kasi pamoja na kiwango cha ujenzi wa mradi huo, ambao utapunguza msongamano wa magari.

Meneja wa mradi wa Darts, Baraka Ally alimweleza Dk. Magufuli kwamba mradi unaendelea vizuri na utakamilika kwa wakati uliopangwa.

Hata hivyo alisema changamoto kubwa inayoukabili mradi huo ni uvamizi wa wafanyabishara ambao wamekuwa wakiweka biashara zao barabarani huku wenye teksi na magari mengine wakiegesha eneo la mradi.

Vile vile alisema kuwa kuna hatari kubwa ya Jiji la Dar es Salaam kukumbwa na harufu kali kutokana na wakazi wanaoishi karibu na barabara kujiunganishia kinyemela mabomba ya maji machafu na mifereji ya mvua.

Magufuli aliagiza watu wote wanaokwamisha mradi huo kuchukuliwa hatua kali, ikiwa ni pamoja na halmashauri kuwajibika katika hilo.


MTANZANIA

WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO- 2013

 
 Muhula wa kwanza kwa wanafunzi wa Kidato cha Tano kuanzia mwaka huu 2013 itaanza mwezi Julai. 


Wanafunzi wamepangwa katika shule zenye miundombinu na walimu kwa masomo husika. 


Aidha, kama baadae upungufu utajitokeza, wakuu wa shule wameelekezwa kufanya taratibu za kuazima walimu wa muda na kutoa taarifa kwa uongozi wa halmashauri husika kuhusu upungufu wa walimu uliopo. 


Kwa nafasi hii, ninaagiza wanafunzi wote kuripoti katika shule walizopangwa tarehe 29 Julai, 2013. Kama kutakuwa na sababu yoyote ya msingi ya kuhamia shule nyingine, uhamisho wa kawaida utafanywa baada ya kuripoti shuleni kupitia kwa mkuu wa shule husika, Mkurugenzi wa Halmashuri/Manispaa na Katibu Tawala wa Mkoa.

 (Wizara haitabadilisha shule walizopangwa wanafunzi)

Wanaporipoti wanatakiwa kuwa na:
   Original Result slip na Living Cerificate


PHILIPO A. MULUGO (MB)
NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
10 Julai, 2013



WASICHANA....<<<  BOFYA  HAPA>>


WAVULANA....<< BOFYA  HAPA>>> 

 >>Ukitaka  kuya  download  bofya  hapo chini

WASICHANA:  << DOWNLOAD>>

WAVULANA:  << DOWNLOAD>>

MWANACHUO WA MWAKA WA KWANZA ALAANI KITENDO CHA KUPIGWA "EXILE" NA MADENTI WENZIE


Vitendo  vya  wanafunzi  kupigana  exile( kumpisha room ili angonoke na mpenzi wake)   vimekuwa  vikishika  kasi  ya  ajabu  katika  hosteli  za  wanafunzi  wa  vyuo  vikuu  mbalimbali ambao  kwao  limekuwa  ni  jambo  la  kawaida...!!

Hali  imekuwa  ni tofauti  kidogo  kwa  mwanafunzi  wa  chuo kimoja  hapa  nchini  ambaye  yuko  mwaka  wa  kwanza na anategemea kuingia mwaka wa pili.


Akiongea  na  mtandao  huu  kwa  sharti  la  kutotajwa  jina , mwanafunzi  huyo  amefunguka  na kudai  kuwa  Exile  imemuathiri  sana  kisaikolojia.Imemfanya  aishi  kama  mtumwa  huku  taaluma  yake  ikiyumba  kwa  kasi.

Hili  ni   simulizi  la  mwanafunzi  huyo:
 
"Maisha ya shule yana changamoto  nyingi sana.Kwa  mtu  yeyote  ambaye  ni  mcha  mungu  ni  lazima  itamuwia  vigumu  sana  kukabiliana  na  hali hii.

"Nasema  hivi  kwa  sababu  ndani  ya  hosteli  huwa  tunaishi  watu   tofauti  wenye malezi  tofauti.Kasheshe  ni  kwetu  sisi  first  year...

"Mazingira  kwetu  ni  mageni  na  ndani  ya  hosteli  tunaishi  na  mabraza  wa  miaka  ya  juu  wenye  wapenzi  wao  hapo hapo chuoni ambao  huwaleta  vyumbani   na  wakati mwngine  hulala  nao.

"Wanapokuja  na  wapenzi  wao  vyumbani  ni  lazima  uwapishe  wafanye  mambo  yao.Na  ukiwapisha  maana  yake  utoke  kwa  zaidi  ya  masaa  matatu  mpaka   matano

"Ndani  ya  chumba  changu  tulikuwa  tunaishi  watatu, mmoja  mwaka  wa  pili, mwingine  wa  tatu  na  mimi  mwaka wa kwanza.Wote  hao  walikuwa  na  wapenzi  wao  hapo hapo  chuoni.

"Siku  zote  za  wikiendi  walikuwa  wamezigawana.Mmmoja  ilikuwa  ni  jumamosi  na  mwingine  jumapili.Yaani  kwa  kifupi  ni  kwamba  sikuwa  na  uhuru wa  kukaa  chumbani   siku za wikiendi  na  wakati  mwingine  hata  siku  za  wiki.

"Nimeamua  niwe  muwazi  maana hali  hii  imekuwa  ni  kero  kwangu   na  imekuwa  ikiniathiri  sana  kisaikilojia  na  kusababisha  taaluma  yangu  iyumbe  nikilinganisha  na  nilipokuwa  naanza.

"Naomba  nitoe  ombi  kwa  wanafunzi wenzangu.Sote  tuko  vyuoni  kutafuta  maisha  na  zile  hosteli  tunazilipia  kwa  gharama  sawa.Kwa  nini  umsumbue  mwenzako  wakati  gesti  zipo?..Yangu  ni  hayo  tu"

HUYO NDO "MELLIS EDWARD" ALIYEKAMTWA NA MADAWA YA KULEVYA AKIWA NA "AGNESS MASOGANGE


Picha  ya  Mrembo Mellis Edward  aliyedakwa  na  madawa  ya  kulevya  Afrika  kusini  akiwa  na  Agness Masogange
Mellis Edward
Inahisiwa kuwa  huyu mwanamke wa pili aliyetajwa na Kamanda Nzowa kwa jina la “Melisa Edward”  ni mdogo wake na Agnes ambaye katika akaunti ya facebook anayo tumia jina la (MELLIS EDWARD) , Agnes amemuweka katika orodha ya family kama ‘sister’ katika akaunti yake ya Facebook.
 Kamanda  Gofrey  Nzowa - Kitengo  cha  Madawa ya Kulevya


 Agness Masogange  akiyahesabu  "MAPESA" yake.Picha  hii aliiweka  siku  chache  zilizopita

"JACK WOLPER ANATAFUTA UMAARUFU KUPITIA JINA LANGU....KAMA SANAA IMEMSHINDA BASI AKAJIUZE AU AKAUZE VIPODOZI"...BABY MADAHA



MWIGIZAJI wa kike na mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Baby Madaha Joseph amemshukia mwigizaji mwenzake wa kike Jack Wolper kwa kudai kuwa amekuwa akitumia vyombo vya habari kumsema na baadae kujifanya anamuomba msamaha huku hana dhamira ya kweli.

Akiongea na FC , msanii huyo amesema kuwa  Jack  Wolper anatumia jina lake ili apande na kuwa Maarufu (nyota ).

“Mimi ni mwanamke mpigaji na ninajua ninachofanya katika maisha yangu...

"Kuna wanawake hawajui misingi ya sanaa.Ni wanawake ambao  wamevamia fani na kutuharibia  sifa  zetu  kama  wasanii..

"Mimi siwezi kugombana na mtu mwenye fani moja ,tena  ya kubebwa . Jack hana cha kufanya akifeli kuigiza labda arudie kazi yake ya kuuza vipodozi...Atafanya nini kingine hapa mjini zaidi  ya  kujiuza?,”alisema Baby Madaha  na  kuongeza:

“Jack anataka kukiki kwa kunichafulia jina langu, lakini mimi ni Star mwenye vision na najua nafanya nini katika Industry..

"Mimi ni kiongozi mtarajiwa .Nategemewa niongoze watu , sasa nikianza kugombana na watu itaniharibia  ndoto zangu za kisiasa,” 

FC

"NASUBIRI WAKATI MWAFAKA WA KUMUONYESHA KIKWETE YA KWAMBA MIMI NI NANI".....HILI NI TISHIO LA KIHUNI LA RAISI KAGAME KWA RAIS KIKWETE


Nikiwa  katika  upekuzi  wangu, nimeshtushwa sana na kauli za  KIHUNI  za Rais  Paul Kagame  dhidi ya  Rais wetu Kikwete na nchi yetu kwa ujumla....

Rais Kikwete ameepuka malumbano na Kagame kwa  kukaa  kimya , lakini inaelekea Kagame  anadhani ukimya wa Kikwete ni uoga kwake  au labda anatafsiri kuwa anadharauliwa.....

Nadhani  huu  ni  wakati  mwafaka  kwetu  sisi  watanzania  kuungana  na  kumuunga  mkono  rais  wetu  juu  ya  huu  UPUMBAVU  wa  Kagame....

Kagame  ni  lazima  atambue  kwamba  watanzania  tupo  tayari  kuilinda  nchi  yetu  kwa  gharama  yoyote  na  kamwe  hatuwezi  kuwa  VIBARKA  wa  Rwanda...

Ifuatayo  ni  Kauli  ya  Kihuni  aliyoitoa  Rais  Kagame  Kwa  Taifa  letu:
-------------------------------------------------------------

.....“Those people [Tanzanian President Jakaya Kikwete] you just heard siding with Interahamwe and FDLR and urging negotiations… negotiations? 


 Me, I do not even discuss this topic, because I will just wait for you [Tanzanian President Jakaya Kikwete] at the right place and I will hit you! He[Tanzanian President Jakaya Kikwete] did not deserve my answer.


 I did not waste my time answering him…It is well known. There is a line you cannot cross, there is a line, a line that you should never cross. It is impossible…”“


It is in these ominous terms that the Rwandan dictator General Paul Kagame threatened to get even with Tanzanian President Jakaya Kikwete, while addressing Rwandan Youth on June 30, 2013 during a summit called “Youth Konnect”“, sponsored by his wife, Janet Kagame.


Relations between Tanzanian President Jakaya Kikwete and Rwandan leaders have soured in the last weeks. On several occasions Rwandan leaders called the Tanzanian President “a genocide and terrorist sympathizer”, “ignorant”, “arrogant”, and “mediocre leader”. 

The relations have deteriorated following the recommendation by President Jakaya Kikwete of open negotiations between Rwandan, Ugandan and Congolese leaders and their respective armed opposition in order to bring durable peace and security in the African Great Lakes region....
 


source..I will Just Wait For You At the Right Place And I will Hit You, Rwandan General Paul Kagame Threatens Tanzanian Jakaya Kikwete

"VYOMBO VYA HABARI HUWA VINAHONGWA NA WAPINZANI ILI VIWAANDIKE VIZURI".....SPIKA WA BUNGE



Spika wa Bunge, Anne Makinda, ameibuka na kauli yenye utata mkubwa akivituhumu vyombo vya habari kwamba vinahongwa na wabunge wa kambi ya upinzani ili viandike habari zao vizuri.

Bila kufafanua ni kwa jinsi gani wabunge hao wanatoa hongo hiyo mbali tu ya kusema wanatoa kitu kidogo ili waandikwe vizuri, pia alikana kuwakandamiza wabunge wa kambi hiyo na kuwabeba wale wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao wako upande wa serikali.

Alisema hana upendeleo katika uendeshaji wa vikao vya Bunge kama anavyoshambuliwa na baadhi ya watu na kwamba lawama zinazoelekezwa kwake zinatokana na watu kuangalia upande mmoja.

Spika Makinda alitoa ufafanuzi huo jana ofisini kwake jijini Dar es Salaam wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari kuhusu vurugu mbalimbali zinazotokea katika vikao vya Bunge mjini Dodoma na hasa juu ya kuporwa au kugeuzwa kwa hoja za upinzani.

Spika Makinda alikuwa ametoka kuzungumza na Spika wa Korea Kusini, Kang Chang Hee.

"Ndiyo najua mnapewa 'kitu kidogo' na hawa wanaoanzisha vurugu bungeni, lakini kusema Spika anapendelea hili siyo kweli hata kidogo,"
aliongeza Spika.

Alisema iwapo angekuwa na kawaida ya kuwakandamiza wabunge wa upinzani kwa kiasi kinachosemwa wengi wa wabunge hao wa upinzani wasingekuwapo bungeni.

“Mimi siwapendelei wabunge wa CCM, ningekuwa hivyo hawa wapinzani wasingekuwapo bungeni,” alisema Makinda muda mfupi baada ya kuzungumza na ujumbe wa Bunge la Korea Kusini uliomtembelea ofisini kwake.

Makinda alisema wakati wa kuendesha vikao vya Bunge haitakiwi kuwa na itikadi za vyama na kwamba kufanya hivyo kunaweza kusababisha vurugu.

Wakati Spika akitoa utetezi huo, wabunge wa upinzani kwa nyakati tofauti wamekuwa wakimtupia lawama za wazi hususani wanapokuwa katika vikao vya Bunge kwamba anawapendelea wabunge wa CCM.

Miongoni mwa mambo ambayo Spika Makinda amekuwa akilaumiwa ni pamoja na kukalia zaidi ya taarifa 10 za ushahidi juu ya kauli za wabunge wa upinzani zilizowasilishwa kwake na yeye kuzikalia kwa muda wote bila kusema lolote.

Miongoni mwa ushahidi huo, umo wa mawaziri kusema uongo bungeni.

Pia Spika amekuwa akilaumiwa jinsi mjadala wa hoja binafsi za wabunge wa upinzani ‘zilivyoporwa’ na serikali, kama ile ya Mbunge wa Kuteuliwa (NCCR-Mageuzi), James Mbatia, kuhusu mitalaa ya elimu; ya mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, kuhusu hali ya upatikanaji wa maji katika jiji la Dar es Salaam, na hata ya Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari, kuhusu ardhi ya Meru.

Zote hizi ama ziligeuzwa na kupoteza maana yake hali iliyosababisha mvutano mkali bungeni ukiacha picha ya upendeleo wa dhahiri kwa baadhi wafuatiliaji wa mijadala ya Bunge.

Akizungumzia mchakato wa kupata Katiba mpya, Spika Makinda alisema Bunge la Katiba litakutana Novemba, mwaka huu na  litawajumuisha wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Baraza la Wawakilishi Zanzibar pamoja na wajumbe 160 ambao hata hivyo alisema sheria haijasema wanapatikana vipi.

Alisema mwezi ujao serikali inatarajia kupeleka muswada wa sheria ili kufanya marekebisho ya namna ya kupata wajumbe hao 160 ambao siyo wabunge.

Spika alisema katika Bunge hilo, yeye hatakuwa mwenyekiti na kwamba wajumbe wenyewe watachagua kiongozi atakayewaongoza.

Kauli ya Makinda iliwahi kusemwa pia na Naibu wake, Job Ndugai, mara baada ya kuahirisha kikao cha Bunge kwenye mkutano uliopita, kufuatia vurugu zilizotokea baada ya hotuba ya Msemaji wa Kambi ya Upinzani Wizara ya Mambo ya Nje, Ezekiah Wenje, kutamka kuwa Chama cha Wananchi (CUF) kina uhusiano na vyama vinavyounga mkono mashoga.

Wakati vurugu zikiendelea nje ya viwanja vya Bunge kwa wabunge wa CUF na Chadema kuzozana, Ndugai alipita ndipo aliulizwa na waandishi Kulikoni, lakini katika hali ya kushangaza, alivituhumu vyombo vya habari kwamba ndivyo vimesababisha hali hiyo.

“Haya yote mmesababisha ninyi waandishi, mnawadekeza sana wabunge wa upinzani, hata wangefanya nini mnawapamba pamba, lakini mkumbuke siku wakiingia madarakani watafanya haya haya wanayofanya leo,” alisema Ndugai bila kufafanua kauli yake.

Kwenye mazungumzo yake na ujumbe wa Bunge la Korea uliomtembelea ofisini kwake, Spika alisema unalenga kudumisha ushirikiano katika nyanja mbalimbali zikiwamo za uwekezaji na kuendeleza uchumi wa nchi hizo mbili.

Kwa upande wake, Spika wa Korea, Chang Hee alisema nchi yake imepiga hatua kubwa ya maendeleo ingawa haina chanzo chochote cha kuzalisha nishati ya umeme ikilinganishwa na Tanzania.

Alisema Bunge la Tanzania linafanya vizuri kwa upande wa nafasi za viti maalum ikilinganishwa na Korea Kusini ambayo idadi ya wanawake bungeni ni ndogo.

MCHUNGAJI MTIKILA AITAKA ZANZIBAR IRUDISHE GHARAMA ZOTE ZILIZOTOLEWA NA SERIKALI YA TANGANYIKA AMBAZO ZIMESAIDIA KUIIMARISHA ZANZIBAR


 Mchungaji Mtikila  amemwandikia  barua  rais Kikwete  akiitaka Zanzibar  irudishe  gharama  zote  za Tanganyika....
Hii  ni  barua  yake:
---------------------------------------------------------
8 July, 2013

HE. MR JAKAYA KIKWETE
PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
STATE HOUSE
DSM

THE RESOURCES OF TANGANYIKA SPENT ON THE UNION AFFAIRS AS FROM 26/4/ 1964 AND HELPED THE ZANZIBARI GOVERNMENT TO DATE



This is to ask you urgently to furnish us with the facts and figures as regards the following:


  1. How much has ever been contributed by each side of the union of Tanganyika and Zanzibar from 26th April 1964 to date, to finance the union services including the ministries of Defense , Home affairs, foreign Affairs, Higher education, etc.

  2. How much has been dished out by our treasury to bail the Zanzaibar Govt out of budgetary constraints, such as payment of the salaries of its government workers or meeting its other emergency requirements.

  3. The cost of Tanganyika's electricity which the state of Zanzibar enjoyed gratis from Tanganyika for all the years.

  4. The amount of finances which our treasury has spent on the Zanzibari parliamentarians in the parliament of Tanganyika (labeled as union parliament), including the expenses on their election, their outfit allowances, their monthly remunerations, their sitting allowances for the bunge sessions, the expenses on their vehicle loans, their medical expenses, their colossal retirement benefits and all other privileges which the Zanzibaris enjoyed from the sweat of the people of Tanganyika in the guise of the "Union".

  5. The amount of money which our treasury has dished out to the political parties and/or Zanzibari politicians, be them under the umbrella of the ruling party or the opposition parties.

Your excellency, the information is urgently required for our extremely urgent public interest moves which are underway, which touch on the inalienable right of the people of Tanganyika to their self determination, which is a basic ingredient of their humanity.

We thank you very much for your anticipated maximum cooperation, which will be very contributory to the consolidation of the independence of the people of Tanganyika and protection of their rightful identity, as much as the people of Zanznibar enjoy these inalienable rights, to the extent of their latest constituonal amendment which amounts to pulling out of the so called "Union", SPARING only the links whoch protect their parasitic advantages which are painful yoke on the neck of our mother Tanganyika, being such a political, economic and social tragedy.

We are by copy of this memorandum asking the accountable ministers and the governor of the central bank which is known to have heavily invested in Zanzibar using Tanganyika's resources, to avail the data as promptly as is required in public intrest.

Rev.Christopher Mtikila

NATIONAL CHAIRMAN (DP)

Copy to:

1.Hon Dr William Mgimwa(Mp), Minister for Finace

2.The Hon.Minister of state in Vice president's office responsible for Union Matters.

3.Hon.Benard Membe (MP) Minister for Foreign Affairs

4.Prof.Benno Ndulu, Governor of the Bank of Tanzania

-via  Wavuti

POLISI YAWAZUIA CHADEMA KUANZISHA KAMBI YA KIJESHI KWA AJILI YA KUWAANDAA VIJANA WAKE



Mnamo tarehe 09/07/2013, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe, Freeman Mbowe alitoa kauli kwamba wanaunda kikundi chao cha kuwalinda ambacho watakipatia mafunzo ya ukakamavu.



Kitendo cha chama chochote cha siasa ikiwemo CHADEMA kuanzisha kikundi cha kujihami ni kinyume cha sheria za nchi na endapo watafanya hivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.



Kufuatia kauli hiyo, Jeshi la Polisi nchini limeanza uchunguzi na litachukua hatua kulingana na ushahidi utakaopatikana. Aidha, Jeshi la Polisi litamshughulikia mtu yeyote atakayekwenda kinyume cha sheria bila kujali wadhifa wake.

Imetolewa na:-

Advera Senso-SSP

Msemaji wa Jeshi la Polisi.

CHADEMA YAJIPANGA KUIMARISHA KITENGO CHA ULINZI NA USALAMA " RED BRIGADE" ILI KUWAKABILI VIJANA WA CCM WATAKAOLETA FUJO


MUHTASARI
Ili kukabiliana na vitendo vya fujo vinavyofanywa na vijana wa CCM dhidi ya wagombea, Wanachama na viongozi wa CHADEMA, Kamati Kuu imeagiza kwamba kitengo cha ulinzi cha Chama “Red Brigade” kiimarishwe zaidi kwa kuhakikisha kuwa vijana wote wa Red Brigade Nchi nzima wanapewa mafunzo maalum ya UKAKAMAVU yatakayoandaliwa katika Makambi maalum katika mikoa yote.
 RIPOTI  KAMILI
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAAMUZI YA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHAMA KILICHOFANYIKA TAREHE 06-07/07/2013 KATIKA HOTEL YA BLUE PEARL, DAR ES SALAAM.

Kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo ilikutana katika Kikao cha dharura kuanzia tarehe 06-07/07/2013 katika Hotel ya Blue Pearl Dar es salaam kujadili pamoja na mambo mengine Rasimu ya Katiba mpya na hali ya Siasa nchini.

Kamati kuu imejadili na kuyatolea maamuzi mambo mbalimbali kama ifuatavyo:

1:0. Hali ya Siasa Nchini.

Kamati kuu imepokea taarifa ya hali ya siasa nchini na kuzingatia mambo yafuatayo:

a) Shambulio la Bomu Arusha.

 Kamati Kuu imesikitishwa na kulaani kwa nguvu zote tukio la Bomu Arusha lililosababisha watu wanne kuuwawa na zaidi ya watu 70 wengine kujeruhiwa vibaya.

 Kamati Kuu imeridhika kwamba shambulio hilo lililenga kuwaua viongozi wakuu wa CHADEMA akiwamo Mwenyekiti wa Taifa Mheshimiwa Freeman A. Mbowe na Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini na Mjumbe wa Kamati Kuu, Mheshimiwa Godbless J. Lema na viongozi na wanachama wengine wa CHADEMA waliohudhuria Mkutano wa kufunga kampeni za udiwani katika Jiji la Arusha pamoja na kuvuruga Uchaguzi huo na kuinyima CHADEMA ushindi mkubwa;

 Kamati Kuu imeridhika kwamba ushahidi uliopo wa vielelezo na wa mashuhuda wa shambulio unaonyesha ushiriki wa moja kwa moja wa Jeshi la Polisi katika shambulio hilo;

 Kamati Kuu imefadhaishwa na kauli ya Serikali bungeni iliyolenga kulikosha Jeshi la Polisi kwa kuhusika kwake na shambulio hilo dhidi ya CHADEMA na wananchi wa Jiji la Arusha na kuilaumu CHADEMA wakati CHADEMA ndio mhanga wa shambulio hilo;

 Kamati Kuu imeshangazwa na kitendo cha Serikali kupuuza maafa yaliyowafika wananchi wa Arusha kwa kushindwa kushiriki katika mazishi ya wahanga wa mauaji ya Soweto na kuwashambulia kwa mabomu ya machozi, vipigo na maji ya sumu waombolezaji waliokusanyika kuwaaga marehemu waliouawa kwenye shambulio;

 Kamati Kuu imesikitishwa na Rais Kikwete kuendelea kukaa kimya juu ya shambulio la Arusha na kushindwa kwake kuunda Tume huru ya Kimahakama kuchunguza kwa uwazi shambulio hilo. Aidha, Kamati Kuu inaamini kwamba ukimya huu wa Rais Kikwete na kushindwa kwake hata kuwatembelea wafiwa na wahanga wengine wa shambulio hilo ni ushahidi mwingine wa kuhusika kwa vyombo vya ulinzi na usalama vya Serikali katika kupanga na kutekeleza shambulio la Arusha;

 Kamati Kuu imefadhaishwa na kitendo cha Bunge la Jamhuri ya Muungano kuendelea na vikao vya Bunge kama kawaida; kukataa kutoa mchango wowote kwa wahanga na kushindwa kupeleka ujumbe wa Bunge kuwatembelea na kuwafariji wahanga na waathirika wa shambulio kinyume na utaratibu uliozoeleka wa Bunge kutambua na kushiriki katika majanga na misiba ya aina hii.

Kamati Kuu inautaka uongozi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano uwaeleze Watanzania kama maafa ya shambulio la Arusha yalikuwa na tofauti yoyote na maafa ya shambulio la bomu la Olasiti, au na maafa ya mabomu ya Gongo la Mboto, ajali ya MV Skargit au maafa mengine yaliyosababisha Bunge la Jamhuri kuahirisha shughuli zake, kutoa michango kwa waathirika pamoja na kupeleka ujumbe wa Bunge kuwafariji wafiwa na wahanga wa matukio hayo;
Kutokana na maelezo hayo hapo juu Kamati kuu imeazimia kuwa:

• Iwapo Rais ataendeleza msimamo wa kutokuunda tume huru ya kimahakama, Ushahidi uliopo juu ya tukio la kurushwa Bomu Arusha utawekwa wazi muda utakapofika kwa wananchi wa Tanzania; vyama na mashirika ya kiraia ya haki za binadamu hapa nchini na ya nje ya nchi; ofisi za kibalozi za mataifa rafiki na Tanzania pamoja na jumuiya ya kimataifa ili yaishinikize Serikali kuunda Tume huru ya Kimahakama kuchunguza shambulio hilo na matukio mengine ya mauaji yenye sura ya kisiasa ambayo yamehusishwa na Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya usalama vya Serikali au vya Chama cha Mapinduzi;


2:0. Hali ya Wananchi wa Mtwara.

Kamati kuu imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa juu ya unyanyasaji, utesaji, ubakaji na uonevu wanaofanyiwa wananchi wa Mtwara hivi sasa na vyombo vya dola huku serikali ikikaa kimya juu ya jambo hili bila kukemea. Kamati kuu imejadili kwa kina namna wananchi wa Mtwara wanavyofanyiwa na vyombo vya dola na kufikia maazimio yafuatayo;

 Vyombo vya dola vitimize wajibu wake wa kulinda amani na mali ya raia na siyo kuwatesa na kuwapiga wananchi kwa kuwasababishia vifo kinyume na Haki za Binadamu.

 Serikali iwasikilize wananchi wa Mtwara na siyo kutumia ubabe, unyanyasaji, uonevu na mateso kama mbinu za kuhalalisha kukubalika kwake kwa wananchi.

 Rais Kikwete alitangazie taifa “hali ya hatari” kwa mkoa wa Mtwara kama anaona kuwa Mtwara ni hatari kwa kiasi hicho cha kulitumia JWTZ kuzunguka mitaani na silaha za kijeshi ili taifa liweze kujua,Aidha kama jeshi la polisi limeshindwa kutimiza majukumu yake kwa mujibu wa sheria atangaze kulivunja jeshi hilo mara moja.

 Serikali iunde tume huru ya kuchunguza matukio ya mauaji,ubakaji,utesaji na ukiukwaji wa haki za binadamu yaliyofanywa na vyombo vya dola na waathirika wote waweze kufidiwa kwa mujibu wa sheria.

3:0. Kauli ya Waziri Mkuu.

Kamati Kuu imejadili kwa kina kauli ya Waziri Mkuu Bungeni kwamba ni sahihi kwa Jeshi la Polisi nchini kuwapiga Wananchi wote wanaotumia haki zao za Kikatiba kupinga sera au maamuzi ya Serikali. Kamati Kuu imeazimia kuwa:

 Kauli ya Waziri Mkuu imekiuka Katiba na sheria za nchi yetu zinazokataza Jeshi la Polisi kutumia nguvu dhidi ya raia wasiokuwa na silaha na ambao wanatumia haki zao za kikatiba kufanya maandamano;

 Kamati Kuu inaamini kwamba kauli ya Waziri Mkuu inatoa Baraka kwa Jeshi la Polisi kuendeleza vitendo vya ukatili na mauaji dhidi ya wananchi ambayo yamelifanya Jeshi la Polisi la Tanzania kutangazwa kuwa moja ya majeshi katili ya polisi katika Afrika Mashariki;

 Kamati Kuu inaungana na wananchi, taasisi na mashirika ya kitaifa na kimataifa ambayo yamelaani vikali kauli hiyo ya Waziri Mkuu na inawataka wananchi, taasisi na mashirika hayo kuendelea kumlaani vikali Waziri Mkuu kwa kauli hiyo;

 Kamati Kuu inaamini kwamba Waziri Mkuu amepoteza sifa za kuendelea kuwa Waziri Mkuu na inaungana na wananchi na taasisi ambazo zimedai Waziri Mkuu awajibike au awajibishwe kutokana na kauli yake hiyo. Aidha, Kamati Kuu inawaelekeza Wabunge wote wa CHADEMA washirikiane na Wabunge wengine wote wenye mapenzi mema na nchi hii na ambao wanaamini katika utawala wa sheria waanzishe mchakato wa kumpigia kura ya kutokuwa na Imani Waziri Mkuu kupitia Bunge;

 Kamati Kuu imewataka Jeshi la Polisi kama sehemu ya jamii ya watanzania kupuuza kauli ya Waziri Mkuu katika utekelezaji wa kazi zao kwa kuwa kauli hiyo ni ya uvunjifu wa Katiba na Sheria na inachochea uvunjifu wa amani.

4:0. Uchaguzi wa Madiwani.

Kamati Kuu imepokea taarifa kuhusu ushiriki wa CHADEMA katika Uchaguzi wa Madiwani uliofanyika tarehe 16/06/2013 katika kata 22.

 Kamati Kuu imeipongeza Sekretarieti na uongozi wa Kanda mbalimbali za CHADEMA kwa maandalizi mazuri katika Uchagzuzi huo uliosababisha CHADEMA kuwapokonya CCM ushindi katika kata 4 ilizokuwa imeshinda katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. Kamati Kuu imewapongeza wananchi kwa kuipatia CHADEMA kura asilimia (47.7%) dhidi ya CCM (49%) na (3.3%) za CUF.

 Kamati kuu imesikitishwa na vitendo vya fujo walivyofanyiwa viongozi, wagombea pamoja na Wanachama mbalimbali katika sehemu mbalimbali palipo fanyika Uchaguzi. Kamati Kuu imesikitshwa na kulaani vitendo hivyo vikiwemo vya watu kukatwa mapanga , kuchomwa visu na kubakwa kwa akina Mama na vijana wahuni walioandaliwa na Chama cha Mapinduzi.

 Kamati Kuu imelaani vitendo hivyo vya kinyama vilivyofanywa mbele ya jeshi la polisi na Wakuu wa Wilaya.

 Ili kukabiliana na vitendo vya fujo vinavyofanywa na vijana wa CCM dhidi ya wagombea, Wanachama na viongozi wa CHADEMA, Kamati Kuu imeagiza kwamba kitengo cha ulinzi cha Chama “Red Brigade” kiimarishwe zaidi kwa kuhakikisha kuwa vijana wote wa Red Brigade Nchi nzima wanapewa mafunzo maalum ya UKAKAMAVU yatakayoandaliwa katika Makambi maalum katika mikoa yote.

 Kamati Kuu imejadili maandalizi ya Uchaguzi wa madiwani katika kata nne (4) katika Jiji la Arusha. Kamati Kuu imepokea kwa masikitiko taarifa juu mipango inayofanywa na jeshi la polisi kwa kushirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo na viongozi wengine wa CCM mkoani Arusha katika kuhujumu zoezi la Uchaguzi kwa kuwatisha wapiga kura kwa kutumia polisi na vijana wa Green Guard siku ya uchaguzi.

 Kamati Kuu inamtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) kuchukua hatua stahiki kuzuia harakati za polisi na CCM za kuvuruga Uchaguzi na kutaka kujipatia ushindi kwa njia za hila. Aidha Kamati kuu imelitaka jeshi la polisi kuheshimu maadili ya uchaguzi yaliyosainiwa na Serikali, Tume ya uchaguzi na vyama vya siasa.

 Kamati Kuu imesikitishwa na Tume ya Uchaguzi kushindwa kuwazuia CCM kuendelea na kampeni za Uchaguzi huku wakiwa wamezuia kampeni hizo kwa vyama vingine.

 Kamati Kuu imeendelea kuwapa pole wananchi wa Arusha kwa matukio mabaya wanaofanyiwa na serikali ya CCM mkoani humo, na imewapongeza kwa kusimama kidete katika kulinda haki na ukweli.

 Kamati Kuu imewaomba wananchi wa Arusha wajitokeze kwa wingi siku ya kupiga kura tarehe 14 Julai 2013, na imewataka wabunge wote washiriki katika kusimamia zoezi la upigaji kura na uhesabuji kura siku ya Uchaguzi na wananchi wajitokeze kwa wingi kulinda kura bila hofu.

5:0. Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kamati Kuu imejadili kwa kina sana maudhui yaliyomo katika Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba;

• Kamati Kuu imetambua kazi kubwa iliyofanywa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika kukusanya na kuchambua maoni ya wananchi na kuandaa Rasimu ya Katiba Mpya;

• Hata hivyo, Kamati Kuu imetambua na kuainisha mapendekezo mengine ya msingi ambayo yanastahili kuboreshwa zaidi katika Rasimu hiyo;

• Msimamo na maazimio ya Kamati Kuu juu ya Rasimu ya Katiba Mpya yameainishwa na kuchapishwa katika kijitabu maalumu ambacho kitazinduliwa katika Mkutano wa hadhara utakaofanyika siku, tarehe na mahali patakapo tangazwa hapo baadaye.


Imetolewa na:

……………………….

Freeman A. Mbowe, (MP)

Mwenyekiti Taifa

Jul 8, 2013

"PREZZO ANAYAJUA MAPENZI.....HATA AKINIUTHI SITAHESABU MAKOSA YAKE"....DIVA WA CLOUDS FM


Muda mfupi uliopita mtangazaji wa ‘Ala za Roho’ ya Clouds FM Diva Loveness Love ambaye sasa anatumia “divathebawse” katika akaunti yake ya Instagram, ameweka picha mpya akiwa na Rapcellency Jackson makini aka Prezzo kutoka Kenya waliyopiga jana (July 7).


Picha hiyo ambayo inawaonesha wawili hao wakiwa “0 distance” ilikuwa na caption inayosomeka hivi,

“Nothing Than Happiness… Prez is such a Nice guy. Hata Akiniudhi Sihesabu makosa yake. May you Live Long Pleaseeee……… Good hearted, My hero, My Mentor… A Person I can count to when I need to be happy… No one is Perfect yes but I love his flaws and All…. Bless you always’ . I Pray you live Long… I Pray for you Always”


Picha nyingine iliwaonesha Prezzo na Diva wakikumbatiana na kusindikizwa na caption “Last Night at escape1… I was nothing than happy. With Prezzo”.




Prezzo alikuwa miongoni mwa wasanii waliotumbuiza jana (July 7) katika show ya Matumaini iliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

SABABU TANO ZILIZOWAFANYA CHADEMA WAGOME KUSHIRIKI "KONGAMANO LA AMANI" LINALOANZA KESHO


Ndugu waandishi wa habari,
Tumewaiteni hapa mchana huu kwa dharula, kutokana na kujitokeza kwa jambo moja muhimu sana katika mustakabali wa chama chetu na taifa kwa ujumla. Jambo lenyewe ni hili:

Kwa muda wa siku mbili, kuanzia kesho– tarehe 9 Julai 2013 hadi 10 Julai – kutakuwa na “KONGAMANO LA AMANI” lililoitishwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania – Tanzania Center For Democracy (TCD).

Kongamano hilo linatajadili na kutafakari Amani ya Taifa, litafanyika kwenye hoteli ya White Sands ya jijini Dar es Salaam. Litafuguliwa na Mwenyekiti wa TCD, Mbunge wa kuteuliwa na Rais, Mheshimiwa James Mbatia na litafungwa na Rais Jakaya Kikwete.

Baadhi washiriki ni pamoja na mawaziri, viongozi wakuu wa vyama vyenye wabunge ambavyo ni wanachama wa TCD – Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chama cha Wananchi (CUF), United Democracy Party (UDP), Tanzania Lebour Party (TLP), NCCR- Mageuzi na Chadema.



Aidha, chama cha UPDP nacho kitashiriki mkutano huo kwa niaba ya vyama vingine ambavyo havina wabunge.

Ndugu waandishi wa habari,
Chadema kikiwa mmoja wa wadau wakubwa wa TCD, kimepokea mwaliko wa kutano huo. Hata hivyo, tunapenda kutumia nafasi hii, kupitia kwenu, kuutangazia umma na wote wanaotutakia mema na kulitakia mema taifa, kwamba hatutashiriki mkutano huo kwa sababu zifuatazo:

Kwanza, Mwenyekiti wa TCD, Mheshimiwa Mbatia kwa makusudi amekiuka maazimio ya kikao ya kuteuwa muwezeshaji wa mkutano huo na badala yake akafungamana na CCM kuteuwa watu anaowataka wao.



Pili, Chadema haitashiriki mkutano huo kwa kuwa Amani haijadiliwi. Amani inatengenezwa na kuwapo kwa mazingira ya haki na usawa; na kwamba aliyebobea katika uvunjaji wa haki hizo, ni serikali yenyewe.

Katika mazingira haya, Chadema inaona hakuna umuhimu wa kushiriki kwenye mkutano ambao washiriki ni wale wale wanaotuhumiwa kuvunja haki za binadamu.



Tatu, Amani siyo ya vyama vya siasa pekee yake. Amani inahusisha wadfau mbalimbali wakiwamo viongozi wa kidini, taasisi za kiraia na mashirika yasiokuwa ya kiserikali. Taarifa zilizopo, ni kwamba mkutano huu haukushirikisha viongozi wa kidini, na hivyo, tunadhani kuwa siyo jambo zuri kama kweli tunataka kutafuta amani ya taifa.

Nne, Chadema haitashiriki mkutano huo kwa kuwa aliyepanga, aliyefadhiri na aliyeitisha mkutano huo kwa mgongo wa TCD, ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, Mizengo Kayanza Peter Pinda, ambaye ndani ya nafasi yake, haonekani kuwa na dhamira ya dhati ya kuwapo amani katika taifa letu.


Ndugu waandishi wa habari;
Ninyi ni mashahidi wa jinsi Waziri Mkuu Pinda alivyo mstari wa mbele katika kuhubiri kauli za chuki, uhasama, uchochezi, ubabe na ukiukwaji wa haki za binadamu nchini.


 Siyo mara moja wala mbili, Waziri Mkuu Pinda amesikika, tena ndani ya Bunge, akihamasiha vyombo vya usalama kuvunja sheria kwa kupiga, kuteka na kung’oa meno watu wanaotumia haki zao za kikatiba kushinikiza serikali kuchukua hatua dhidi yamaovu.

Tano, Chadema haitashiriki katika mkutano huo kwa kuwa Serikali ya CCM inayofadhiri mkutano huu, imejaa unafiki kwa kuhubiri amani mchana, wakati usiku inachochea uhasama wa kidini, kisiasa na inawagawa Watanzania kwa misingi ya imani za kidini na vyama.
 


Chadema inao ushahidi usio na chembe ya mashaka, kwamba mifarakano mingi inayotokea kwenye jamii, mapigano katika koo mbalimbali, ugomvi wa kugombea ardhi kati ya wakulima na wafugaji, machafuko kwenye mikutano ya hadhara ya vyama vya upinzani, sababisho kuu ni CCM kuvitumia vyombo vya dola, kutaka kukibeba chama hicho.

Tunataka umma utuelewe, kwamba tuna dhamira ya dhati ya kuona Tanzania inakuwa kisiwa cha amani, lakini hatutakubali kushiriki katika vikao ambavyo wanaoviongoza hawana dhamira hiyo.


 Ili amani iweze kupatikana, ni sharti tuwe kuwepo mijadala inayoingia kwenye viini vinavyosababisha amani ikosekane na hatua hiyo ianze kuchukuliwa na ione inachukuliwa na serikali.

Chadema kiko tayari, kufanya kazi ya kutafuta amani na wale wanaopenda demokrasia. Chadema haifanyakazi na wanafiki wa amani.

Imetolewa na:
Benson Singo Kigaila,
Mkurugenzi wa Oganaizesheni ma Mafunzo,
Dar es Salaam

MASANJA MKANDAMIZAJI AFICHUA UBAGUZI WA BANK YA CRDB KATIKA UTOAJI WA AJIRA


Katika  upekuzi  wangu  , niliamua  kumtembelea  masanja  mkandamizaji  kuona  alichokandamiza  jioni  hii...

Hii  ni  post  yake  facebook  iliyofichua  UBAGUZI  wa  bank  ya  CRDB  katika  utoaji  wa  ajira  kwa  wasomi  wetu  hapa  nchini...

------------------------------------------------------------------------

Internship opportunities with CRDB Bank PLC. These opportunities cover different regions/branches all over the country as indicated below.
•Arusha
•Bagamoyo
•Bukoba
•Dar es Salaam
•Geita
•Ifakara
•Karagwe
•Kigoma
•Kilombero
•Makambako
•Mbeya
•Morogoro
•Njombe
•Shinyanga
•Singida
•Songea
•Tabora

Minimum Requirements
Final year student from UDBS also other UDSM Students will be considered
•GPA of at least 3.5
•The applications should comprise CVs, Provisional results, a cover letter indicating the station/branch of preference among the mentioned above.

Due to limited space only shortlisted candidates will be contacted.

Deadline: 10th July, 2013 at 1500hrs

Submission: online (career@udbs.udsm.ac.tz) or B.324 (office hours)

SWALI: TANZANIA KUNA VYUO VIKUU VINGAPI?
------------------------------------------------------------------------