Apr 21, 2013

Matumaini ya makubaliano ya Kongo na M23 yafutika

Imeelezwa kuwa, matumaini ya kufikiwa makubaliano baina ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na waasi wa M23 yamefutika kufuatia hatua ya Umoja wa Mataifa ya kubadilisha jukumu la askari wa kofia bluu wa umoja huo huko Kongo. Gazeti la Potentiel la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo linaripoti kwamba, hatua hiyo ya Umoja wa Mataifa imepunguza uwezekano wa serikali ya nchi hiyo kutiliana saini makubaliano ya amani na waasi wa Machi 23. Kwa mujibu wa azimio nambari 2098 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa askari wa kofia bluu wa Umoja wa Mataifa sasa wana ruhusa ya kufanya operesheni za kijeshi dhidi ya waasi  wa M23 na kwa msingi huo wameondoka katika nafasi yao ya kuwa askari wa kulinda amani na kuwa vikosi vya kupambana na waasi. Hatua hiyo ya Umoja wa Mataifa imetajwa kuwa imefuta kabisa uwezekano wa kufikiwa makubaliano ya amani baina ya waasi wa M23 na serikali ya Kinshasa. Aidha wiki iliyopita Uganda ilishindwa kuikurubisha pamoja mitazamo ya waasi wa M23 na wawakilishi wa serikali ya Kinshasa katika mazungumzo ya Kampaka.

No comments: