Jun 21, 2011

KUNDI LA UNDERZONE NDIYO WASHINDI KATIKA SERENGETI DANCE LA FIESTA 2011.

Kundi la Underzone kutoa jijini Dar es Salaam limeweza kunyakua taji katika shindano la Serengeti Dance la Fiesta 2011 lililofanyia Maisha Club jijini Dar es Salaam ambapo ameyabwaga chini makundi mawili la Kontejazz kutoka jiji Arusha pamoja na MYUT kutoka mji kasoro Bahari. Kundi hilo liliweza kupokea hundi ya shilingi milioni moja pamoja na zawadi kibao kwenye picha hapo juu unaweza kuona jinsi washindi hao walivyokua na furaha baada ya kunyakua ushindi huo uliokua una mtihani mkumbwa................................................

Majaji wa shindano hilo la B-12 ambaye ni mtangazaji wa Clouds Fm 88.4 jijini Dar es Salaam akiwa na muandaaji wa kipindi cha ‘Step Up Player’ Isakwisa Thomson wakijaribu kumnyamazisha Msami kutoka T.H.T ambaye alianza kulia kabla ya kutangaza matokeo jambo ambalo lilionyesha ni jinsi gani asivyopenda watu washinde kufanya vyema.

Mc wa shindano hilo Babuu wa Kitaa ambaye ni mtangazaji wa Clouds Tv akiongea na wanaikundi cha Underzone baada ya kumaliza kuonyesha umahili wao.

Hakika ilikuwa ni vuta nikuvute maana kila kundi lilionyesha umahili wa ucheza na muonekano wa mavazi pia.

UB-40 kutoka Zanzibar nao hawakuwa nyuma kuwasha moto.


Adamu Mchomvu ambaye ni mtangazaji wa Clouds Fm na pia ni msanii wa bongflava  anayetamba na nyimbo yake ya John! John! akiwasha moto ndani ya Maisha Club ambapo alisindikiza fainali ya shindano la Serengeti Dance la Fiesta 2011.

No comments: