Jun 1, 2013

KIBAKA ACHOMWA MOTO HUKO MBAGALA BAADA YA KUIBA BEGI NA SIMU.....


Jamaa  akimmalizia mtuhumiwa kwa  tofali...
 Kibaka  mmoja  amejikuta  akiyaaga  maisha ya  uraiani  baada ya   kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali....

Tukio hili limetokea maeneo ya mbagala charambe mida ya saa sita mchana baada ya kibaka huyu kuingia  ndani ya nyumba ya mtu na kuiba begi...

Taarifa zinaeleza kwamba, raia mwema ambaye ni mkazi wa nyumba hiyo alisahau kufunga mlango  na  kwenda kwa jirani...Alipotoka tu, Kibaka huyo alizama   ndani na kuchukua begi la nguo taratiiibu kama lake! 

Hakuridhika na begi,  alivyotazama pembeni aliona kuna  simu .Bila  kupoteza muda, kibaka huyo aliihifadhi mfukoni ..

Balaa  liliazanza wakati anajiandaa  kutoka...Alipofika  mlangoni, kibaka huyo alikutana na mwenye nyumba uso kwa uso.....!!! 

SINEMA ILIANZIA HAPO!!!!! Watu mwiziii... mwiziiii mwiziiiiiiiiiii....!!!!! 

Kutokana na uzoefu wake wa muda mrefu, jamaa huyo alibahatika kujisweka ndani  jumba bovu lililoko uchochoroni na kuinusuru roho yake....

Raia wenye hasira kali hawakumuona wakapita, Kufika mbele kidogo walikata tamaa. Wakati wanarudi nyumbani kwao mara ghafla  jamaa  akakurupuka na  kuchomoka kwenye dirisha la lile jengo bovu alikokuwa amejificha....
 
Harakati zikaanza upyaaaaaa!!!!! YAAAANI...!! jambazi hakuchukua raundi akatiwa mikononi... 

MPENDWA msomaji,   mambo yalienda kama tunavyoona hapo pichani.
Moto unawaka!
 Tairi limeletwa
Mwizi  amevishwa tairi na kutiwa moto!

masaimbofu

No comments: