HATIMA
ya filamu ya mwigizaji, Vincent Kigosi ‘Ray’, Sister Mary iliyokuwa
imezuiwa kwa kudaiwa kudhalilisha ukatoliki, imefahamika kuwa mwigizaji
huyo amesalimu amri ya viongozi wa kanisa hilo.
Cover la filamu hiyo ya Sister Marry.
Baadhi ya vipande vilivyomo katika filamu hiyo.
Akipiga stori na mwandishi wetu, Ray amebainisha kuwa baada ya
kuambiwa achomoe vipande vingi kwenye filamu hiyo, ameona ni bora
kuachana nayo kwani hata akitoa haitaleta maana hivyo atakujairudia upya
wakati mwingine. “Asilimia 85 ya filamu niliigizia kanisani na ndivyo walivyosema niviondoe, sina ujanja kwa sasa nimeanza kushuti filamu nyingine kabisa ile labda nije kuirudia upya hapo baadaye,” alisema Ray.
No comments:
Post a Comment