Apr 27, 2013

HUYU NDIO KIJANA AMBAYE AMEFUKUZWA HUKO SAUDI ARABIA KUTOKANA NA KUWA HANDSOME KUPITA KIASI..


Huyu ni Omar Borkan Al Gala, mwigizaji na pia mpiga picha wa huko Dubai ambaye kwa mujibu wa taarifa, yeye pamoja na wenzake wawili wamefukuzwa huko Saudi Arabia kutokana na kuwa na muonekano mzuri kupitiliza
(Yaani ma-handsome kupita kiasi) ili kuepusha kuwaingiza katika tamaa wanawake ambao hushindwa kujizuia kuwashobokea.


Omar alitolewa na maafisa wa polisi na kunyimwa kuhudhuria katika tamasha ambalo hufanyika kila mwaka nchini humo ambalo huusisha mbio za Ngamia, Janadriyah Festival ambalo kwa sehemu kubwa huhudhuriwa na matajiri, na baadhi ya vyanzo vya taarifa vinasema Omar alitolewa kutokana na mualiko wa msanii wa kike maaruku kutoka Falme za Kiarabu ambaye walihofia angeweza kutengeneza mahusiano naye.... na wengine wakisema ni hofu ya wakubwa kuibiwa mademu wao. 


CHANZO : THESWAGAZONE BLOG

No comments: