May 16, 2013

BREAKING NEWSSSSSSSSS.POLISI MSTAAFU AMCHARANGA MWANAE WA MIAKA 4 KWA MAPANGA .SAMAHANI MSOMAJI KWA BAADHI YA PICHA UTAKAZOZIONA.



ASKARI POLISI MSTAAFU SAMSON BWIRE AKIWA AMEFIKISHWA HOSPITALINI MDA MCHACHE BAADA YA KURUKA KUTOKA KWENYE GARI AKIJARIBU KUKIMBIA.
KAHAMA.
Mkazi wa kitongoji cha Sango kata ya Nyasubi wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga Samson Bwire (54), anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kumcharanga mapanga mtoto wake Devotha Gerald (4) kwa sababu za wivu wa kimapenzi.
Tukio hilo limetokea leo jioni nyumbani kwa Bwire baada ya kuanza kugombana na mke wake Happiness Elius (28)  huku akiwa amelewa pombe ambapo, mkewe alikimbia kitu kilichosababisha kumgeukia mtoto Devotha na kuanza kumkata mapanga kichwani.
Kwa mujibu wa majirani, kelele zilisikika kutoka kwenye mji huo na kwamba walipoenda walimkuta Bwire akichoma nguo za mke wake, na alipowaona aliingia ndani na kuanza kumkata mapanga mtoto huyo huku akiwa amefunga mlango.
Imefafanuliwa kuwa, baada ya kusikia kelele za mtoto, majirani walianza kuvunja milango huku wakiomba msaada kituo cha Polisi na baada ya Polisi kufika walifanikiwa kumnusuru mtoto akiwa amejeruhiwa vibaya sehemu za kichwani.
Majirani kwa hasira walianza kumpiga Bwire ambaye ni askari polisi mstaafu wa cheo cha koplo kwa nia ya kumwua, hali ambayo imelipa jeshi la Polisi kazi ya ziada kumnusuru na kumpakia kwenye gari kwenda kituoni.
Hata hivyo Wakati gari la Poisi likiwa katika mwendo wa kasi eneo la soko la Mkulima, Bwire ameruka kutoka kwenye gari na kuangukia kwenye Lami kitendo kilichomsababishia majeraha makubwa sehemu za usoni.
Mtoto Devotha na baba yake Bwire wote wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kahama kwa matibabu huku Bwire akiwa Chini ya Ulinzi mkali wa polisi.

MATUKIO KATIKA PICHA
 
MTOTO WA MIAKA 4 DEVOTHA GERLAD ALIYEKATWA MAPANGA NA BABA YAKE,HAPA AKIWA HOSPITALI KWA HUDUMA AYA KWANZA.
  
WANANCHI WAKIWA NJE YA HOSPITALI YA WILAYA WAKIWA NA SHAUKU YA KUMUONA MTUHUMIWA.

KINA MAMA WALIOGUSWA NA TUKIO WAKIWA NJE YA HOSPITALI KUMUONA MTOTO HUYO.

AFANDE BWIRE AKIWA HOI WODINI

HAPA AFANDE AKIWA HOI BAADA YA KUFIKISHWA HOSPITALINI..

MADAKTARI WAKIJITAHIDI KUOKOA MAISHA YA MTOTO HUYO.

MADAKTARI WAKIWA KAZINI KUHAKIKISHA WANAOKOA MAISHA YA MTOTO HUYO.

AFANDE BWIRE AKIWA HOI WODINI HUKU AKIWA AMEFUNGWA PINGU.

JITIHADA ZA KUOKOA MAISHA YA MTOTO ZIKIENDELEA

INASIKITISHA SANA JAMANI

MAJUKUMU YA KUOKOA MAISHA YA MTOTO HUYO YAKISONGA KWA KASI.

AFANDE BWIRE AKIWA NA PINGU ZAKE WODINI

MWANDISHI NA MMILIKI WA BLOG HII AKIWA WODINI KIKAZI

MUNGU AMPE AHUENI MTOTO HUYU.
source:kijukuublog

No comments: