Apr 21, 2013

BARAZA LA VIJANA CHADEMA JIMBO LA KAHAMA LANENA KUHUSU HUJUMA YA UCHAGUZI WA MABARAZA YA KATIBA KAHAMA..

MWENYEKITI WA BAVICHA KAHAMA SHIJA BENEDICT

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO – CHADEMA

JIMBO LA KAHAMA, S.L.P 922 KAHAMA

                                        BARAZA LA VIJANA JIMBO LA KAHAMA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI (PRESS RELEASE)

HUJUMA NA UKIUKWAJI MKUBWA WA TARATIBU ZA KUWAPATA WAJUMBE WA MABARAZA YA KATIBA YA WILAYA/HALMASHAURI YA MJI-KAHAMA

                CHADEMA jimbo la Kahama,Kupitia Barazala la Vijana Chadema-BAVICHA Kahama, inapenda kuufahamisha  umma wa Kahama na Watanzania wote kuwa; Tumesikitishwa sana na hujuma zilizofanywa na CCM wilaya ya Kahama chini ya uratibu wa katibu wao wa wilaya Bw. Michael Charles katika mchakato mzima wa upatikanaji wa mabaraza ya katiba ya wilaya.
Ndugu Wanahabari na Watanzania wenzangu, 
Kwanza, Miongoni mwa hujuma hizo ni pamoja na kuwatisha watendaji  na kuwashurutisha kufuata maelekezo ya CCM,Yaliyohusu wagombea wanaotakiwa na CCM  na si wanaotakiwa na Wananchi,katika mpango huo CCM iliwaita vitongoji wote, wenyekiti wa mitaa kuwapa majina manne yaliyopitishwa  na kamati za siasa za kata za CCM katika wilaya ya Kahama.
                Pili, katika maeneo ambayo Hakuna Vitongoji wakuchaguliwa au Wenyeviti wa mitaa, CCM ili kuainisha nafasi hizo kwa watu ambao hawakuchaguliwa na wananchi kinyume na Sheria ,Hata pale Wananchi na Wagombea  walipo hoji watendaji wa kata waliwapuuza kwa hofu ya vitisho toka CCM.
                Tatu ,katika maeneo ambayo Mpango  wa CCM ulipuuzwa na Vitongoji au Wenyeviti wa mitaa ,ilihali idadi kubwa ya Vitongoji,Wenyeviti wa mitaa wakitokana na CCM,CCM iliwaamuru watendaji kupeleka karatasi za kura katika ofisi ya CCM Wilaya ili kutambua ni akinani walio saliti mpango huo,Eti kwa kile kinachoitwa hatua za kinidhamu za kichama,Watanzania,kitendo cha kutambua kura hizo ni uhalifu,umafia na hujuma kwani kura hizo zilikuwa za siri na kwa vyovyote vile ni kinyume cha sheria na Taratibu za Tume ya Maoni ya Katiba,kutoa siri za kura,pia ni uchochezi na hatari kwa usalama wa wahusika.
                Nne ,Ni wazi kuwa Wenyeviti  wa mitaa/vitongoji  walikuwa na wajibu wa kupigia kura Wananchi, baada ya kuwahoji  na kupima uwezo wao wa kujadiliana  kupambanua mambo  kupitia maelezo na wasifu wa Wagombea/Waombaji, kitendo kilichofanywa na vitongoji katika kata ya Nyihogo kwa wao kama Wenyeviti kugombea nafasi za ujumbe huku wakiwa na (interest) katika W.D.C hakikubaliki na ni unyimaji wa haki kwa wananchi wasio na “interest”na Baraza la maendeleo la kata (W.D.C), moja kwa moja.Pia kitendo cha kupitisha majina ya watu ambao hawa kuhojiwa wala kutoa maelezo,  ilikupima uwezo wao ni uvunjaji wa taratibu,nani hujuma,CCM katika hili imefanya na inafanya umafia, kinacho shangaza nikuachwa kwa kundi kubwa la Wasomi na Wataalamu wa Fani mbalimbali ikiwemo,wasomi wa sheria,badala yake na kwa-misingi ya Kisiasa, Umafia na Uhuni wa CCM Wajumbe takribani  asilimia 80% ni Darasa la saba na hawajui chochote kuhusu Katiba,ila kungoja maelekezo toka CCM,,Huu ni Umafia na Uhuni wa makusudi dhidi ya Watanzania,hasa Wanakahama.
                Tano,  kitendo cha mtendaji wa kata ya Mhongolo kutoshughulikia malalamiko ya wagombea kabla ya zoezi la kuwahoji kuanza,juu ya uhalali wa kitongoji cha NYAMHELA kuwakilishwa  na mtu ambaye hakuchaguliwa na wananchi Bw.Amos Jikala kwa maelekezo ya CCM, Huku ni kunyima Haki, Uchochezi na matumizi mabaya ya ofisi ya umma kwa mujibu wa sheria za Nchi. BAVICHA kwa niaba ya CHADEMA  Jimbo la Kahama  tunaomba wananchi watuunge mkono katika hatua zote  zitakazo chukuliwa na CHADEMA Taifa juu ya Umafia na Hujuma ya CCM kwa Watanzania.
                Sita, Kitendo cha kihuni kilichofanywa na mtendaji wa kata ya MHONGOLO Bw. Emmanuel Kalolo ,kuchakachua maamuzi ya W.D.C (Baraza la Maendeleo la Kata),kwa kubadili muhtasari  tena ndani ya ofisi ya CCM  Wilaya ya Kahama  na kuwasilisha majina katika ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji,majina yaliyoelekezwa  na CCM,Yasiyo tambuliwa na W.D.C   na ambayo Diwani kama mwenyekiti  wa W.D.C hakusaini,kitendo cha kubandika majina ya washindi katika mbao za matangazo  na kisha kuandika muhtasari wenye majina mengine ni Umafia,Uchochezi, Unyimi wa Haki na matumizi mabaya ya ofisi za Umma.
                Saba, kitendo chakaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Bw. Felix Kimario, kutumiwa na CCM kufaniksha Umafia wao,Ni kinyume na sheria, Watanzania !!! Baada ya watendaji waadilifu kwa Umma kukataa maelekezo ya CCM katika mkakati wao wa kimafia wa kuhujumu Maoni na maamuzi ya Wananchi , CCM walitumia ofisi ya kaimu Mkurugenzi ,kwa kutuma baadhi ya maafisa wa Umma kutekeleza mpango wa kihatifu wa CCM.Hata baada ya watendaji hao waadilifu kushikilia misimamo na miiko yao ya kazi ,kaimu Mkurungenzi huyu wa Halimashauri ya Mji wa Kahama ,aliamua kuangiza Watendaji hao waadilifu kutoa nyakara mbalimbali zinazohusu zoezi hilo ikiwemo kura za siri.Eti kwa utambuzi katika ofisi za CCM Wilaya ,Huu ni Uhuni,Umaifa ,Unyimi wa Haki na matumizi mabaya ya ofisi ya Umma.
Hitimisho, Baraza la vijana Jimbo la Kahama kwa niaba ya Chadema Jimbo la Kahama tuna laani vitendo hivyo vya kihuni,Kimafia ,Unyimi wa Haki na Matumizi mabaya ya Madaraka na Ofisi za Umma.Ninachukua wasaha huu kuwaomba  wana kahama na Umma wa Watanzania kutuunga mkono katika kila hatua, Itakayochukuliwa na Chadema Taifa kwa maslahi ya Taifa, Ya leo na ya kizazi  kijacho.

Watanzania CCM ni Janga la Kitaifa, Tuwamwage -2014/2015.

Source Kijukuu Blog

No comments: