Mar 15, 2013

ULIMBUKENI WA SOCIAL NETWORK



YULE denti wa chuo kimoja jijini Mwanza ambaye wiki iliyopita tuliandika habari ya picha zake za utupu kuzagaa kwenye mtandao wa BBM, Fatuma Omari amejikuta kwenye wakati mgumu kufuatia madai kuwa familia yake imemtenga.
 
Chanzo chetu kilichoomba hifadhi ya jina lake kilidai kuwa, mara baada ya kutoka kwa habari hiyo, baadhi ya ndugu zake walikasirika na  kutaka kujua undani wake.
“Ile stori ilipotoka ndugu wa Fatuma hawakuamini kuwa kweli kapiga picha hizo.

“Kwa bahati kuna mtu aliyekuwa na picha hizo, walipoziona, waliumia sana na baadhi wakafikia hatua ya kusema hawana radhi naye,” kilidai chanzo hicho.

Ijumaa lilimtafuta Fatuma ili kuzungumzia madai hayo bila mafanikio ila kijana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Saleh baada ya stori kutoka, alipigia simu  na kusema:

“Fatu ni mdogo wangu, nashangaa mmemuandika kuwa kapiga picha chafu wakati siyo kweli. Kama hizo picha zipo nitakuja kuziona laa sivyo tutapelekena mahakamani,” alisema Saleh.

Tumeamua kutumia picha hiyo chafu hapo juu aliyopiga Fatuma ili kuonesha uhalisia.
CREDIT : GPL

No comments: