SHARO MILLIONEA KUZIKWA LEO.......
Kuhusu kifo cha msanii/mwigizaji
Sharo Milionea, namkariri Kamanda wa Polisi Tanga akisema “leo majira ya
saa mbili usiku kwenye barabara ya Segera Muheza mtu mmoja
alietambulika kwa jina la Hussein Ramadhani au Sharo Milionea akiwa
anaendesha gari namba T478 BVR Toyota Harrier akitokea Dar es salaam
kwenda Muheza alipofika eneo hilo gari lake liliacha njia na kupinduka
mara kadhaa na kusababisha kifo chake, mwili wa marehemu umehifadhiwa
kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza”
Kamanda amesema hakuna kona kali sana
wala ubovu wa barabara kwenye sehemu aliyopata ajali Sharo Milionea,
katikati ya Segera na Muheza ambapo gari imehifadhiwa mahali salama kwa
sababu haitembei.
Kwenye gari alikua
mwenyewe.
No comments:
Post a Comment