Jan 7, 2011

Diva ashobokea kutembea mapaja nje!

Presenta wa programu ya Ala za Roho inayovunja mawingu kupitia Kituo cha Redio cha Clouds FM, Loveness Malinzi ‘Diva’ anapenda kuvaa nguo za kihasara hasara, amefunguka.

Diva ameeleza hayo ikiwa ni siku chache tangu alipopiga picha zilizoonesha sehemu kubwa ya maungo yake nyeti ya mwili wake kama ilivyoripotiwa na gazeti hili.

Akitupia maneno katika ‘blogi’ yake, Diva alisema kuwa, mara nyingi anapenda asilimia kubwa ya mwili wake kuwa wazi hivyo kulazimika kuvaa aina hiyo ya nguo.

No comments: