Jun 14, 2012

WAIGIZAJI WA FILAMU WAFURAHIA KUFANYIKA KWA TUZO ZA FILAMU MWAKA HUU


Mwigizaji wa filamu Irene Uwoya akiongea mbele ya waandishi wa habari katika mkutano wa kutangaza tuzo za filamu zinazotarajiwa kufanyika hapa nchini TUZO hizo  za kwanza kabisa za waigizaji wa filamu zimepangwa kufanyika mwezi ujao, Mratibu wa kampuni ya Bantu Film Award, Stuart Kambona amesema, Mkutano huo umefanyika leo kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es salaam. Mwigizaji Irene Uwoya amewapongeza waandaaji hao kwa kuanzisha tuzo hizo ambazo alisema zitawapa changamoto kwao kuandaa filamu za ushindani.
Alishukuru kampuni ya Bantu kwa kuanzisha tuzo hizo ambazo anaamini zitawafanya  kuandaa filamu zenye ubora wa hali ya juu.


Waandishi wa habari wakiadika mambo muhimu yalioongelewa katika mkutano huo
Mwigizaji Rich Mtambalike naye alipata nafasi ya kuzungumza machache katika mkutano huo na kushukuru waandaji kwa kuanzisha tuzo hizo ambazo zitatoa nafasi kubwa kwa waigizaji wa filamu, waandishi wa filamu na waongozaji wa filamu kujitangaza kitaifa na kimataifa
Mwigizaji Jacob Steven akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano huo

Tuzo za Filam kufanyika mwezi ujao


Na Mwandishi Wetu
TUZO za kwanza kabisa za waigizaji wa filamu zimepangwa kufanyika mwezi ujao, Mratibu wa kampuni ya Bantu Film Award, Stuart Kambona alisema leo.
Kambona alisema kuwa hatua ya kuanzisha tuzo hizo inatokana na muitikio wa soko la filamu za Tanzania kwa hivi sasa tofauti na awali. Alisema kuwa Watanzania wengi walikuwa wanapenda zaidi filamu za kigeni na kufunika zile  za hapa nyumbani.
Alisema kuwa kutokana na mapinduzi yaliyofanywa na wasanii wa fani hiyo, filamu za Tanzania kwa sasa zina soko la hali ya juu na imtokana na tabia ya watanzania kubadili mwelekeo. Alisema kuwa ili kuhakikisha Tanzania inafikia hatua ya Hollywood, wameamua kutoa tuzo kwa wasanii waliofanya vizuri na kuifikisha  fani hiyo katika hatua ya sasa.
“Tunaamini kuwa kupitia tuzo hizi, waigizaji au wasanii wa filamu watatengeneza filamu zenye ubora wa hali ya juu ili kuweza kutwaa tuzo na soko kwa ujumla, tunaamini tutafikia lengo letu japo tumebakisha muda  mfupi mpaka tuzo zenyewe kufanyika,” alisema Kambona.
Alisema kuwa kwa kuanzia watashindanisha filamu zote za Tanzania ambazo kwa sasa zipo sokoni ili kutoa fursa kwa kila msanii wa fani hiyo kushindana.  Jumla ya tuzo 28 zitashindaniwa kwa mwaka huu.
Baadhi ya tuzo hizo ni Filamu Bora, Muongozaji Bora, Muigizani Bora mkuu wa Kiume, Muigizaji Bora Mkuu wa Kike, Msaidizi Bora Mkuu msaidizi wa kike na wa kiume, msanii chipukizi bora, filamu ya asili, Mpiga picha bora, Best Sound Track, Best Make-Up artist, Best Costume Designer, Best Documentary, Best Visual effect, best Film editor,  best script na Tuzo ya Heshima.
Tuzo nyingine ni Outstanding Pioneer, Best Comedian, Best Cover Design, Best producer, Best Distributor, Best Action Movie, Best African Film outside Tanzania, Best Ligting, Best Sound na Best Story.
Muigizaji nyota wa kike nchini, Irene Uwoya aliwapongeza waandaaji hao kwa kuanzisha tuzo hizo ambazo alisema zitawapa changamoto kwao kuandaa filamu za ushindani.
Alishukuru kampuni ya Bantu kwa kuanzisha tuzo hizo ambazo anaamini zitawafanya kuandaa filamu zenye ubora wa hali ya juu.
"Tuzo hizi zitatufanya tufanye kazi nzuri zaidi ili kuingia katika ushindani, natoa wito kwa waigizaji wenzangu kufanya kazi kwa umakini ili kuleta msisimko na ushindani zaidi," alisema Uwoya.
Muigizaji Mkongwe, Jacob Steven (JB) alisema kuwa anaamini tuzo hizo zitawafikisha pale ambao wao wamekusudia na vile vile kuibua vipaji vingine katika tasnia hiyo.
JB alisema kuwa tuzo hizo zitawafanya mashabiki wao kujua undani wa fani yao kwa kuwajua watunzi bora, wapiga picha bora na wengineo.

No comments: